Romans 3:1-6

Uaminifu Wa Mungu

1Basi kuna faida gani kuwa Myahudi? Au kuna thamani gani katika tohara? 2 aKuna faida kubwa kwa kila namna! Kwanza kabisa, Wayahudi wamekabidhiwa lile Neno halisi la Mungu. 3 bIngekuwaje kama wengine hawakuwa na imani? Je, kutokuamini kwao kungebatilisha uaminifu wa Mungu? 4 cLa hasha! Mungu na aonekane mwenye haki, na kila mwanadamu kuwa mwongo, kama ilivyoandikwa: “Ili uthibitike kuwa wa kweli unaponena,
na ukashinde utoapo hukumu.”

5 dIkiwa uovu wetu unathibitisha haki ya Mungu waziwazi, tuseme nini basi? Je, Mungu kuileta ghadhabu yake juu yetu ni kwamba yeye si mwenye haki? (Nanena kibinadamu.) 6 eLa hasha! Kama hivyo ndivyo ilivyo, Mungu angehukumuje ulimwengu?
Copyright information for SwhKC